Mwongozo wa Nguu Za Jadi: Guide & Summary Notes

23982 views 273 downloads.

Riwaya inaanza na Mangwasha akiwa na wanawe wawili, Sayore na Kajewa, katika kanisa fulani, ambapo yeye na watu wengine wa kabila lake la Waketwa wamekimbilia usalama baada ya kuchomewa nyumba zao katika eneo la Matango.Kuna fununu kwamba jamii ya Waketwa inafukuzwa kutoka makwao kwa sababu kuna watu fulani wanaotaka ardhi ya Matango kwa nguvu.Mtemi Lesulia, kiongozi wa nchi, anachukia kabila la Waketwa kwani anatoka katika kabila la Wakule.Waketwa na Wakule wana uhasama wa tangu jadi. 

Mangwasha ni msichana mwenye bidii kazini, katika afisi ya Chifu Mshabaha.Anakutana na Mrima, ambaye pia ni mwenye bidii, na kuchumbiana.Wanafanya mazoea ya kwenda kula chakula katika mkahawa unaomilikiwa na Sagilu, mzee ambaye ni rafikiye Mtemi Lesulia.Sagilu anamtaka Mangwasha kimapenzi na anapomkataa, anaweka kisasi dhidi yake.Siku ya harusi ya Mangwasha na Mrima, Sagilu anamtuma Sihaba, kimada wake, na bomu ambalo linalipuka na kusababisha watu waliohudhuria sherehe kutawanyika.Baada ya miaka kadhaa katika ndoa na kuwa na watoto wawili, Mrima anabadilika. Anaitelekeza familia yake na kuingilia ulevi.

Waketwa ni watu wenye bidii.Hata hivyo, wengi wao wanaishia kufanya kazi duni na wanabaguliwa kwa kila hali kwani utawala wa Mtemi Lesulia ni fisadi na unaendeleza ubaguzi dhidi yao.Kuna matatizo ya kiuchumi yanayotokana na uongozi mbaya; vijana waliosoma hawana ajira na wengi wao hawasomi kutokana na umaskini uliokithiri.Pia, kuna uharibifu wa mazingira kutokana na mapuuza na kutojali kwa serikali.Uhalifu umeongezeka na maadili kuwakimbia watu, hasa vijana.Lonare anamtembelea Mangwasha.Tunafahamu kwamba machifu wamelazimishwa kuwahamisha Waketwa kutoka Matango ili Mtemi Lesulia asipate upinzani katika eneo hilo, na Lonare asichaguliwe, kwani wafuasi wake wengi wanaishi huko.Baadaye, Sagilu anamtembelea Mangwasha usiku na kutaka kumhonga kwa pesa ili amkubali. 

Sura hii inaanza asubuhi baada ya watu kukesha nje ya kanisa.Hii ni baada ya kufurushwa kutoka Matango.Mangwasha na Mbungulu wanakutana na wanawake wengine ambao wanaelezea kwamba usiku walipochomewa nyumba walikutana na vijana.Hawa walikuwa na magaleni yaliyohanikiza harufu ya mafuta ya petroli.Vijana hao waliingia kwenye gari jekundu lililoendeshwa na mwanamke fulani ambaye hawakuweza kumtambua. Mkurugenzi wa ardhi mjini Taria anakuja mahali pale akiandamana na Chifu Mshabaha na mwanamke aitwaye Mbwashu.

Nchi ya Matuo inakaribia uteuzi wa viongozi.Sagilu, aliyekuwa na matumaini makubwa ya kupata uteuzi wa kugombea uongozi wa Matango, anapata msururu wa mapigo.Ana uhusiano wa kimapenzi na mpenzi wa mwanawe, Mashauri, aitwaye Cheiya.Mashauri anapogundua jambo hili, anamchukia babake hata kumkana. Zaidi ya hayo, anajiunga na kundi linalomuunga mkono Lonare na Mwamba, ambao wanawania kiti cha mtemi na uongozi wa eneobunge la Matango mtawalia.

Siku chache kabla ya uchaguzi mkuu, Lonare anaripotiwa kupotea.Hata hivyo, wafuasi wake wanaamua watampigia kura, awepo au asiwepo.Hii ni licha ya Mtemi Lesulia kusema kwamba kiti cha mgombea nafasi ya mtemi katika Chama cha Ushirika kifutiliwe mbali kwani Lonare mwenyewe hayupo.Asubuhi ya siku ya uchaguzi mkuu, Lonare anapatikana ametupwa nje ya nyumba ya Mangwasha akiwa katika hali mahututi.Wafuasi wake waliokuwa wameishiwa na matumaini wanajitokeza kwa wingi kwenda kumpigia kura huku mwenyewe akipelekwa hospitalini.Lonare anachaguliwa mtemi wa nchi ya Matuo.Baada ya ushindi huu, anaihutubia nchi. Ahadi anazotoa za kubadilisha nchi na kuleta maendeleo.

Get the Complete and Detailed Guide PDF for Only Ksh 100.00 Ksh 250.00. Includes Plot Summary, Characters & Characterization, Themes, and Stylistic Devices.

Enter your details below to initiate a payment using MPESA.

Please fill out this field.
Looks good!
Looks good (optional field)!
Attachments can be downloaded immediately after purchase, and a copy will also be sent to your provided email.

🛒 Save Time! Add this item to your cart, shop more, and pay for everything at once—quick, easy, and hassle-free!

Continue Shopping

Access more guides and notes for Nguu Za Jadi

Nguu Za Jadi Muhtasari & Maudhui

Muhtasari wa Nguu za Jadi

Price: Ksh 80.00 Ksh 200.00

Maudhui Katika Nguu za Jadi

Price: Ksh 80.00 Ksh 200.00

Nguu Za Jadi Section Summaries and Notes

Nguu Za Jadi Sura Ya Kwanza Notes

Price: Ksh 30.00 Ksh 80.00

Nguu Za Jadi Sura Ya Pili Notes

Price: Ksh 30.00 Ksh 80.00

Nguu Za Jadi Sura Ya Tatu Notes

Price: Ksh 40.00 Ksh 100.00

Nguu Za Jadi Sura Ya Nne Notes

Price: Ksh 40.00 Ksh 100.00

Nguu Za Jadi Sura Ya Tano Notes

Price: Ksh 40.00 Ksh 100.00

Nguu Za Jadi Sura Ya Sita Notes

Price: Ksh 40.00 Ksh 100.00

Nguu Za Jadi Questions and Answers

Nguu Za Jadi Questions and Answers

Price: Ksh 100.00 Ksh 250.00

0